Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 47 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 392 2019-06-18

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA (K.n.y. MHE. MARTHA M. MLATA) aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga vizuri barabara za Kibaya - Urughu, Urughu – Mtekente na Mtekente – Ndago zilizopo Wilayani Iramba ili kufungua fursa za kiuchumi kwa wananchi wa eneo hilo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Martha Moses Mlata, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara za Kibaya – Urughu, Urughu – Mtekente – Kisonga na Mtoa – Kisonga – Ndago yenye urefu wa kilometa 61.46 zimekuwa zikifanyiwa matengenezo kwa nyakati tofauti ili kuhakikisha zinapitika nyakati zote.

Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 barabara ya Kibaya – Urughu ilifanyiwa matengenezo ya sehemu korofi kwa urefu wa kilometa 16 kwa gharama ya shilingi milioni 40.8 na pia barabara ya Mtoa – Kisonga – Ndago ilifanyiwa matengenezo ya muda maalum kwa urefu wa kilometa sita na makalvati matatu yalijengwa. Katika mwaka wa fedha 2017/2018 barabara ya Urughu – Mtekente – Kisonga ilifanyiwa matengenezo ya sehemu korofi kwa urefu wa kilometa 12.5 kwa gharama ya shilingi milioni 53.3.

Mheshimiwa Spika, vilevile katika mwaka wa fedha 2018/2019, jumla ya shilingi milioni 188.8 zimetengwa kwa ajili ya kujenga box culvert kubwa la midomo miwili katika Mto Mtekente, kazi ya ujenzi imeanza na inatarajiwa kukamilika mwezi Agosti, 2019. Aidha, katika mwaka wa fedha 2019/2020 kupitia TARURA barabara ya Urughu – Mtekente – Kisonga imetengewa kiasi cha shilingi milioni 224.3 kwa ajili ya ujenzi wa box culvert kubwa katika Mto Kisonga na barabara ya Mtoa – Kisonga – Ndago imetengewa kiasi cha shilingi milioni 18 kwa ajili ujenzi wa kufanyiwa matengenezo ya sehemu korofi kwa urefu wa kilometa sita.