Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 47 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 391 2019-06-18

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:-

Halmashauri nyingi zina uwezo mdogo wa kujiendesha kwa kutumia mapato yake ya ndani.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutenga fedha katika bajeti ili kuzisaidia Halmashauri kujenga hospitali na vituo vya afya badala ya kuziachia jukumu hilo Halmashauri pekee?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikitekeleza mkakati wa ujenzi, upanuzi na ukarabati wa vituo vya kutolea huduma za afya kwenye Halmashauri mbalimbali nchini. Katika mwaka wa fedha 2017/2018 na mwaka 2018/2019 Serikali imejenga, imekarabati na kupanua vituo 352 ikiwa hospitali tisa, vituo vya afya 304 na zahanati 39 vya kutolea huduma za afya nchini kwa gharama ya shilingi bilioni 184.67.

Mheshimiwa Spika, vilevile katika mwaka wa fedha 2018/2019 Serikali imetoa kiasi cha shilingi bilioni 100.5 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa hospitali 67 za Halmashauri. Aidha, katika mwaka wa fedha 2019/2020 Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 10.4 kwa ajili ya ujenzi wa vituo 52 vya afya na shilingi bilioni 46.5 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali 27 za Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha na kujenga vituo vya afya vya kutolea huduma kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.