Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 44 Energy and Minerals Wizara ya Madini 371 2019-06-12

Name

Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:-

Serikali ilituma wataalam wa madini, mazingira na maji katika Kijiji cha Sakale, Tarafa ya Amani kuangalia uwezekano kama uchimbaji wa dhahabu unawezekana katika maeneo hayo.

Je, Serikali imefikia uamuzi gani kuhusu suala hilo?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Balozi Adadi Mohamed Rajab, Mbunge wa Muheza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tarehe 02/10/2018 timu ya wataalam wa madini, mazingira na maji kutoka Ofisi ya Tume ya Madini Tanga, Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, wataalam wa Bonde la Mto Zigi, Maafisa Misitu na Serikali ya Kijiji walitembelea na kukagua eneo la Kijiji cha Sakale na Kiara ili kuangalia athari za uchimbaji uliokuwa unafanywa na wachimbaji wadogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya ukaguzi, timu ya wataalam ilibaini uharibifu mkubwa wa mazingira uliofanywa katika vyanzo vya maji na Msitu wa Amani na hivyo shughuli za uchimbaji madini zilisitishwa katika eneo hilo ili kunusuru mazingira, vyanzo vya maji na Msitu wa Amani. Katika kusaidia utunzaji wa mazingira, Mradi wa Matumizi Endelevu ya Ardhi katika Bonde la Mto Zigi unaendelea na unafadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Kimataifa (UNDP) kwa kushirikiana na Wizara ya Maji kwa manufaa ya sasa kwa wananchi na vizazi vijavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, natoa wito kwa wachimbaji wadogo wa Tarafa ya Amani kuangalia maeneo mengine nje ya Bonde la Mto Zigi ili kufanya shughuli za uchimbaji.