Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 44 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 366 2019-06-12

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM aliuliza:-

Mwaka 2019 kutafanyika uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa mujibu wa sheria.

Je, Serikali ina mkakati gani unaoendelea katika maandalizi ya mchakato wa uchaguzi huo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Masoud Abdallah Salim, Mbunge wa Jimbo la Mtambile kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuhakikisha uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2019 unafanyika kwa ufanisi, Serikali imekamilisha maandalizi ya Kanuni za uchaguzi zitakazotumika kuendesha uchaguzi huo. Kanuni hizo zimetangazwa katika Gazeti la Serikali la tarehe 26 Aprili, 2019 kwa kupewa namba kama ifuatavyo:-

(i) Tangazo la Serikali Namba 372 kuhusu Kanuni za Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Mtaa na Wajumbe wa Kamati ya Mtaa katika mamlaka za Miji.

(ii) Tangazo Namba 371 linalohusu Kanuni za Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kitongoji katika Mamlaka za Miji.

(iii) Tangazo Namba 373 linalohusu Kanuni za Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kijiji, Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji na Mwenyekiti wa Kitongoji katika Mamlaka za Wilaya na

(iv) Tangazo Namba 374 linalohusu Kanuni za Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kijiji, Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji na Mwenyekiti wa Kitongoji katika Halmashauri za Miji.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Serikali imehakiki maeneo ya utawala na kufanya mafunzo na mikutano kwa wadau wa uchaguzi huo. Vilevile Serikali inaendelea na maandalizi ya ununuzi wa vifaa vya uchaguzi na imetenga kiasi cha shilingi 82,975,994,000.148 Kwa ajili ya kuendesha uchaguzi huo. Ahsante.