Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 42 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 348 2019-06-10

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA (K.n.y. MHE. CATHERINE V. MAGIGE) aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha mchakato wa ulipwaji fidia kwa wananchi zaidi ya 2,000 wa Wilaya ya Longido na Monduli ambao maeneo yao yalipitiwa na Mradi wa Umeme Vijijini (REA)?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Catherine Valentine Magige, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini inatekeleza mradi wa kupelea umeme katika vijiji vyote nchini ifikapo mwezi Juni, 2021. Lengo la mpango huu ni kuhakikisha kuwa Watanzania zaidi ya asilimia 85 wanatumia umeme ifikapo mwaka 2025. Ili kuhakikisha lengo hili linafikiwa, Serikali inagharamia miundombinu, ujenzi na gharama ya kufikisha huduma hii ya umeme kwa wananchi kwa asilimia 100 na wananchi kulipa shilingi 27,000 tu ikiwa ni Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ya huduma hiyo. Hivyo, miradi ya umeme vijijini haina fidia.

Mheshimiwa Spika, naomba kutumia fursa hii kuwaomba wananchi wa Longido, Monduli na Watanzania wengine kutoa ushirikiano katika utekelezaji mradi huu ikiwa ni pamoja na kutodai fidia, nakushukuru.