Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 41 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 339 2019-06-03

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA aliuliza:-

Mkoa wa Dodoma una mahitaji ya walimu 11,676 kwa uwiano wa 1:40 kwa shule za msingi. Kwa sasa walimu waliopo ni 7,382 na hivyo kuwa na upungufu wa walimu 4,410 sawa na asilimia 38.

Je, ni lini Serikali itaajiri mwalimu wa kutosha Mkoani Dodoma?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA W. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI,naomba kujibu swali la Mheshimiwa Felister Bura, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dodoma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikiajiri na kuwapanga walimu kwenye Halmashauri kwa awamu. Kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2017/2018 na 2018/2019 Serikali imeajiri walimu 14,422 ambapo 10,695 ni walimu wa shule za msingi na 3,727 ni walimu wa shule za sekondari. Mkoa wa Dodoma umepatiwa walimu 699 wa shule za msingi kati ya walimu 10,695 walioajiriwa wa shule za msingi. Serikali itaendelea kuajiri walimu kwa awamu kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.