Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 38 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 319 2019-05-29

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:-

Je, Serikali imejipangaje kutekeleza mojawapo ya malengo katika Mpango wa Maendeleo wa miaka 5 kwa Taifa 2016/2017, 2020/2021 katika kupanua wigo wa Utalii nchi (diversification)?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amina Saleh Mollel, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika kupanua wigo wa mazao ya utalii, Wizara kwa kushirikiana na wadau wa utalii inaendelea na jitihada za kuendeleza mazao mbalimbali ya utalii na kutangaza ikiwemo; kuanzisha mradi wa utalii wa utamaduni kwenye maeneo mbalimbali nchini; utalii wa fukwe kwa kuanzisha kurugenzi itakayosimamia uendelezaji wa utalii huo nchini; utalii wamali kale kwa kuimarisha vitu mbalimbali vya mali kale, pamoja na kuimarisha utalii wa mikutano na maonesho (Meetings Incentives Conference and Events-) kwa kuboresha muundo wa Bodi ya Utali(TTB) utakaowezesha kuwa na kitengo kinachosimamia utalii huo, pamoja na kufanya tathmini ya ujenzi wa kumbi za mikutano katika eneo la Pwani la Bagamoyo na Dar es Salaam, na utalii wa meli kubwa za kitalii (Cruiseship Tourism) ambapo tunashirikiana na Mamlaka ya Bandari kuboresha miundombinu ya bandari ili kukidhi mahitaji ya utalii huo nchini pamoja na kuendeleza utalii wa Jiolojia katika Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo, Wizara imeanzisha shughuli mpya za utalii zikiwemo; safari za puto (Hot air balloon) katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha; utalii wa kutembea katika kamba(canopy walkway) katika Hifadhi ya Taifa Manyara; Utalii wa kuzoesha Sokwe (habituated chimpamzees) katika Hifadhi ya Taifa ya Rubondo pamoja na kuimarisha na kutangaza Hifadhi za Misitu ya Asili nchini ili kuvutia watalii kutembelea maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, Wizara imeanza kutekeleza Mradi wa Resilient Natural Resource Management for Tourism and Growth (REGROW) ambao kazi zake ni kuendeleza na kutangaza vivutio vya utalii, kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika Sekta ya Utalii pamoja na kuboresha miundombinu inayozunguka katika vivutio vya utalii vilivyopo Nyanda za Juu Kusini ikiwemo barabara na viwanja vya ndege. Ni imani yangu kuwa, utekelezaji wa mradi huu utasaidia ukuaji wa Sekta ya Utalii katika Ukanda wa Nyanda za Juu Kusini sambamba na kupanua wigo wa mazao ya utalii katika utalii katika Ukanda wote wa Kusini kwa ujumla.