Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 38 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 316 2019-05-29

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Primary Question

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE aliuliza:-

Serikali inafanya juhudi katika kuendeleza elimu hapa nchini kwa kutoa elimu bure na hata kujenga Shule nyingi zikiwemo za kata.

Je, lini sasa Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kukamilisha Maabara za Sayansi katika Shule zote za kata nchini?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMIESEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Prof. Jumanne Abdallah Maghembe, Mbunge wa Mwanga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mpango wa ujenzi wa maabara za masomo ya sayansi katika shule za sekondari kwa kushirikisha wananchi na wadau wa maendeleo wa ndani na nje. Katika mwaka wa fedha 2019/ 2020, Serikali imetenga kiasi cha jumla shilingi bilioni 107.1 zikiwemo shilingi bilioni 58.2 kupitia mpango wa lipa kulingana na matokeo (EP4R) na shilingi bilioni 48.9 kupitia mgango wa kuboresha shule za sekondari (SEQUIP) ambapo sehemu ya fedha hizo zitatumika kukamilisha ujenzi wa maabara za masomo ya sayansi kwa shule za sekondari za kata nchini. Ahsante.