Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 37 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 315 2019-05-28

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za ujenzi wa jengo jipya la kisasa la Askari Polisi wa Makunduchi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, Mbunge wa Viti Maalum kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua changamoto ya uhaba wa nyumba za makazi ya askari katika eneo la Makunduchi na katika Mkoa wote wa Kusini Unguja. Eneo la Makunduchi lina jengo moja la ghorofa la makazi ya familia nne za askari lililorithiwa toka Serikali ya Mkoloni na Mahanga mawili yanayotumiwa kwa makazi ya askari. Makazi haya ni sawa na asilimia 10 tu ya mahitaji halisi. Kwa kutambua changamoto hii, Serikali imeanzisha ujenzi wa nyumba za makazi ya familia 12 za askari polisi katika Mkoa wa Kusini Unguja. Aidha, Serikali kwa kupitia jeshi la polisi na kushirikiana na wadau imeanzisha ujenzi wa kituo cha polisi cha Daraja B huko Dunga, kituo hiki kimefikia hatua za mwisho kumalizika.