Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 37 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 312 2019-05-28

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:-

Vijiji vya Sintali, Nkana, Nkomachindo na Katani viko kwenye mpango wa kupata umeme wa REA Awamu ya III lakini mpaka sasa hakuna kazi zinazoendelea:-

Je, ni lini kazi hiyo itaanza?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Desderius John Mipata Mbunge wa Nkasi Kusini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, jumla ya vijiji 51 vitapatiwa umeme katika Wilaya ya Nkasi ikiwa ni pamoja na vijiji 12 vya Jimbo la Nkasi Kusini vya Ntuchi, Tambaruka, Chima, Chatelekesha, Isasa, Kingombe, Ntemba, Nkomolo II, Kasapa, Kisula, Namansi na Kasu B. hadi kufikia mwezi Mei, 2019 umeme tayari umeshawasha katika vijiji vya Chala, Chima, Chala Isasa na Ntemba. Jumla ya wateja wa awali 77 wameunganishiwa umeme. Aidha, mkandarasi anaendelea na kazi katika vijiji 9 viliovyosalia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi za mradi katika Jimbo la Nkasi Kusini vinahusisha ujenzi wa kilometa 29.65 za njia ya umeme wa msongo kilovoti 33; kilometa 28 za njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4; ufungaji wa transfoma 14 na uunganishwaji wa wateja wa awali 324. Gharama za kazi hiyo inakadiriwa kufikia shilingi bilioni 2.15.

Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vya Sintali, Nkana, Katani na Nkomachind vitapatiwa umeme kupitia mradi wa REA III mzunguko wa pili unatarijiwa kuanza mwezi Julai, 2019 na kukamilika mwezi Juni, 2021.