Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 37 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 311 2019-05-28

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-

Serikali aliahidi kupeleka umeme katika vijiji vyote vya Jimbo la Mbulu Vijijini kupitia REA III kwa sababu REA II haikufanya vizuri katika jimbo hilo:-

Je, vijiji vingapi vitafikiwa na umeme wa REA Awamu ya III?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay Mbunge wa Mbulu Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imedhamiria kufikisha umeme katika vijiji vyote visivyo umeme nchini ifikapo Juni 2021. Jimbo la Mbulu Vijijini lina vijiji vipatavyo 76 na kati ya vijiji hivyo 12 vimepatiwa umeme. Vijiji 13 vya Qaloda, Getesh, Endesh, Labay, Maretadu, Hayderer, Endanachan(Haydom), Muslur, Dirim, Simha, Yaeda Ampa, Endoji na Gidhim vimejumuishwa katika mradi wa REA III mzunguko wa kwanza. Mkandarasi Kampuni ya Angelique International Limited kutoka India anaendelea na kazi za kusambaza umeme katika Jimbo la Mbulu Vijijini. Kazi ya kupeleka umeme katika vijiji vilivyopelekewa umeme zitakamilika mwezi Juni, 2020.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi zinazoendelea kwa sasa ni pamoja na kusimika nguzo, kuvuta nyaya na kufunga transfoma katika Vijiji vya Qaloda, Getesh, Endoji, Endesh, Labay, Maghang Juu, Getagujo na Simahha. Kati ya vijiji hivyo, vijiji 6 vya Getesh, Endoji, Qaloda, Labay, Getagujo na Maghang Juu vitawasha umeme mwisho wa mwezi Mei, 2019. Kazi za mradi zinahusisha ujenzi wa kilometa 45.87 za njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 na kilometa 35 za njia ya umeme wa msongo kilovoti 0.4, ufungaji wa transfoma 16 na uunganishaji wa wateja wa awali 347 na gharama za mradi ni shilingi bilioni 2.6.

Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vilivyobaki katika Jimbo la Mbulu vitapatiwa umeme kupitia mradi wa REA III mzunguko wa pili utakaoanzwa kutekelezwa mwezi Julai, 2019 na kukamilika mwezi Juni, 2021.