Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 37 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 308 2019-05-28

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza:-

Je, kuna utaratibu wowote wa kuajiri watu wote waliohitimu Vyuo na kukidhi vigezo vya kuajiriwa?

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani Mbunge wa Viti maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa muda mrefu Serikali imekuwa Mwajiri Mkuu, wa Wahitimu wa Vyuo mbalimbali kutoka katika soko la Ajira nchini. Ajira hizi zimekuwa zikitolewa kwa kuzingatia mahitaji halisi ya raslimali watu katika Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala na Taasisi mbalimbali za Serikali kwa kuzingatia ikama na bajeti iliyotengwa kwa ajili ya kugharamia ajira mpya katika Utumishi wa Umma.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na mabadiliko ya kijamii na kiuchumi, Serikali ilianzisha Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma, kwa lengo la kuratibu mchakato wa ajira katika Utumishi wa Umma kwa uwazi na ushindani kwa njia ya usaili wa nadharia na vitendo pale inapobidi. Hivyo, wahitimu wanaofaulu usaili ndiyo wanaokidhi vigezo vya kuajiriwa na huwa wanaajiriwa kwa kada zote.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba Duniani kote, Serikali siyo mwajiri pekee wa wahitimu wa vyuo mbalimbali vya elimu, kwani pamoja na kuajiriwa Serikalini, wahitimu hao huajiriwa pia katika Sekta binafsi, Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali, Asasi za Kiraia na maeneo mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, wahitimu wengine huamua kujiajiri wenyewe na hivyo kutoa mchango wa maendeleo kwa Taifa kwa njia moja au nyingine. Aidha, kuhitimu Elimu ya juu, siyo kigezo pekee cha kuwezesha muhitimu husika ila sifa na ushindani wa kutosha ili kuweza kuajiriwa na Serikali. Hivyo, Serikali haina utaratibu wa kuajiri wahitimu wote wa vyuo vya Elimu ya juu nchini. Ahsante.