Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 31 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 258 2019-05-20

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI aliuliza:-

(a) Je Ikama ya Wataalam wa Ardhi Katika Halmashauri za Wilaya ni ipi na ni lini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru itafikia kiwango hicho?

(b) Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kurudisha eneo la Hekari takribani 2,000 za Shamba Pori la Nambarapi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ili nayo irejeshe ardhi kwa Wananchi wa Vijiji husika kikiwemo Kijiji cha Nambarapi?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-

Mheshimimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Ramo Makani Mbunge wa Tunduru Kaskazini lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimimiwa Spika, kwa mujibu wa viwango vya utendaji vya mwaka 2015, ikama ya Wataalam wa ardhi katika Halmashauri za Wilaya Maafisa Ardhi watatu, wanatakiwa Wapima Ardhi watatu, Maafisa Mipangomiji watatu, Wathamini watatu na Mafundi Sanifu Upimaji pamoja na Maafisa Ardhi Wasaidizi wanne. Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru kwa sasa ina watumishi wanne katika Sekta ambao ni Maafisa Mipangomiji wawili, Mpima Ardhi mmoja na Afisa Ardhi Msaidizi mmoja. Serikali inaendelea kutenga fedha kila mwaka kwa ajili ya watumishi wa Sekta ya Ardhi ili kufikia kiwango kinachohitajika na hivyo kuongeza ufanisi. Aidha, Wizara itawapanga upya watumishi wa Sekta ya Ardhi ili kuwa na uwiano wenye tija.

Mheshimimiwa Spika, sehemu ya (b) ya swali lake shamba hili linatambuliwa kama “Shamba Namba 69 Nambarapi” na lina ukubwa wa hekta 774 ambazo ni sawa sawa na (ekari 1,913). Mwaka 2003 kulianza kujitokeza migogoro wa kugombea ardhi ya shamba hili hali iliyosababisha kufunguliwa kwa Shauri namba 03 la mwaka 2016 katika Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya ya Tunduru. Shauri hili lilikuwa kati ya TAMCU Ltd dhidi ya wananchi wanne (Hassan Mussa Ismaili, Ismail Mussa Ismail, Sophia Mussa Ismail na Said M. Ndeleko. Katika Shauri hili Chama cha Ushirika Wilaya ya Tunduru kilipata ushindi. Pamoja na ushindi wa TAMCU Ltd, wananchi wa kijiji cha Nambarapi waliomba ardhi katika shamba hilo kwa TAMCU ambapo ekari 1,000 zilimegwa na Mrajisi wa Vyama vya Ushirika na kugawa kwa wananchi. Hivyo, sehemu ya shamba iliyobaki ni mali ya chama cha Ushirika Wilaya ya Tunduru yaani (TAMCU Ltd).