Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 100 2019-09-12

Name

Eng. Joel Makanyaga Mwaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chilonwa

Primary Question

MHE. JOEL M. MWAKANYAGA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuitengeza barabara inayounganisha kijiji cha Bwawani kilichopo Kata ya Manchali na Kijiji cha Ikowa kilichopo Kata ya Ikowa ili iweze kupitika katika kipindi chote cha mwaka?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshmiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joel Mwaka Makanyaga, Mbunge wa Chilonwa, kama ifuatavyo:-

Mheshmiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Wilaya ya Chamwino imekuwa ikifanya matengenezo ya mara kwa mara ili kuwezesha barabara hiyo kupitika nyakati zote. Katika mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali ilifanyia matengezo barabra ya Chinangali II – Ikowa yenye urefu wa kilomita tatu kwa gharama ya shilingi milioni 14.15.

Mheshimiwa Spika, ili kuifikia barabara ya Chinangali II – Ikowa ni lazima kutengeneza kwanza barabara ya Mwegamile – Makoja - Ikowa na katika mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali imetenga kiasi cha shilingi milioni 114 kwa ajili ya kufanyia matengezo barabara ya Mwegamile –Makoja – Ikowa. Aidha, tathmini iliyofanywa na Wakala wa Barabra za Vijiji na Mijini (TARURA) imebainisha kuwa jumla ya shilingi milioni 668.2 zinahitajika kufanya matengenezo makubwa ambayo ndiyo itakuwa suluhisho la kudumu kwenye barabara ya Ikowa - Kiegea kwa maana ya Bwawani yenye urefu wa kilomita 12.3.

Mheshimwia Spika, katika mwaka wa fedha 2018/ 2019, Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino imetengewa bajeti ya shilingi bilioni 1.4 kwa ajili ya matengenezo ya barabara na ilipokea kiasi cha shilingi bilioni 1.2 ikiwa ni asilimia 82 ya bajeti. Baadhi ya barabara zilizotengenezwa ni barabara ya lami ya Chamwino Mjini, Haneti – Kwahemu- Gwandi na Zajilwa. Chinangali II – Chilowa na barabara ya Dabalo – Segela. Aidha, kwa mwaka fedha 2019/2020 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino imetengewa kiasi cha shilingi bilioni 1.366 kwa jili ya matengenezo ya barabara.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na jitihada za kutafuta fedha kuiwezesha TARURA kuimarisha mtandao wa barabara wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino ikiwa ni pamoja na barabara inayounganisha Kijiji cha Bwawani – Ikowa.