Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Madini 98 2019-09-11

Name

Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Primary Question

MHE. JANET Z. MBENE Aliuliza:-

Geological Surveys za Wilaya au Mikoa mingi ni za miaka mingi tangu enzi za ukoloni. Surveys hizi nyingi zimejikita kwenye aina moja ya migodi kwa mfano Mkoa wa Songwe Survey imezungumzia machimbo ya mawe peke yake:-

(a) Je, ni lini Serikali itafanya mapitio ili kupata Geological Surveys zenye kujumuisha aina nyingine za madini ambayo yanapatikana katika Mkoa wa Songwe hususan Ileje?

(b) Je, Serikali ipo tayari kwenda kuwaelimisha wananchi wa Ileje juu ya madini yaliyopo na kuhamasisha uwekezaji kwa wachimbaji wadogo?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI Alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Janet Zebedayo Mbene, Mbunge wa Ileje, lenye vipengele (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Serikali kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imekuwa ikifanya tafiti mbalimbali za jiolojia kwa ajili ya kuainisha madini mbalimbali yaliyopo nchini tangu kipindi cha mkoloni hadi sasa. Aidha, GST kwa ushirikiano na ufadhili wa Serikali ya Jamhuri ya watu wa Korea imeanza kufanya utafiti wa kina wa kijiolojia ili kuongeza na kuboresha taarifa za uwepo wa madini mengine katika Mkoa wa Songwe na mikoa mingine nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tafiti zilizofanyika Mkoa wa Songwe zinaonesha kuwa Wilaya ya Ileje ina madini yafuatayo; moja ikiwa ni madini ya metali aina ya dhahabu yanayopatikana katika maeneo ya Mwalisi na Ikinga, Madini ya Viwandani aina ya Ulanga, yanayopatikana katika maeneo ya vilima vya Bundali na Ileje, madini ya nishati aina ya makaa ya mawe (Coal) yanapatikana katika maeneo ya Songwe, Kiwira na madini ya apatite na niobium yanayopatikana katika miamba ya carbonatite iliyopo maeneo ya kilima cha Nachendazwaya, ikiwa ni pamoja na madini mengine kama marble na madini mengine ya ujenzi.

(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania itaendelea kufanya tafiti mbalimbali za madini katika Wilaya ya Ileje na maeneo mengine ya nchi kwa kadri ya upatikanaji wa rasilimali ya fedha na kutoa elimu kwa wananchi juu ya upatikanaji wa madini katika maeneo mbalimbali ya nchi ikiwa ni pamoja na kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya madini kwa wachimbaji wadogo.