Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 93 2019-09-11

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY Aliuliza:-

Katika mradi wa REA I na II vijiji vingi vya Jimbo la Mbulu Mjini havikufikiwa na umeme na katika vijiji vilivyofikiwa ni kaya kati ya 20 mpaka 30 pekee ndizo zilizopata umeme:-

(a) Je, ni lini REA III itapeleka umeme katika Vijiji 26 vya Jimbo la Mbulu Mjini?

(b) Awamu ya I na II ziliruka shule nyingi, vituo vya afya na Makanisa. Je, ni lini sasa taasisi hizo zitapelekewa umeme?

(c) Je, ni lini Serikali itarudia usambazaji wa umeme katika vijiji vyote vilivyosambaziwa sehemu ndogo sana katika Jimbo la Mbulu Mjini?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI Alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini, lenye sehemu (a), (b) na (c), kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utekelezaji wa Mradi wa REA III, Mzunguko wa Kwanza katika Jimbo la Mbulu Mjini, jumla ya Vijiji vitatu vya Gwaami, Tsaayo na Banee vitapatiwa umeme na Mkandarasi Kampuni ya Angelique International Limited.

Aidha, vijiji vitatu vya Murray, Silaroda na Gunyoda vinaendelea kupelekewa umeme na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kwa Mpango wa Umeme Vijijini. Vijiji 20 vilivyobaki vya Jimbo la Mbulu Mjini vya Hereabi, Maheri, Kuta, Qwam, Nahasey, Hayasali, Hasama, Hayloto, Kwermusi, Amowa, Gwandumehhi, Aicho, Gedamar, Qalieda, Laghanda mur, Gidamba, Qatesh, Landa, Tsawa na Jaranja vitapatiwa umeme kupitia mradi wa REA III, Mzunguko wa Pili unatarajiwa kuanza Januari, 2020.

(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, shule, vituo vya afya na taasisi nyingine ambazo hazijaunganishwa umeme katika vijiji au maeneo ya karibu yaliyounganishwa umeme na miradi ya awali ikiwemo REA I na II yatapelekewa umeme katika kipindi hiki. Tumetoa wito kwa Halmashauri au taasisi husika zilipie gharama za kuunganisha umeme ili taasisi hizo ziunganishiwe umeme.

(c) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maeneo ya Mbulu Mjini yaliyosambaziwa umeme, tunawaomba wananchi wa maeneo ya karibu na maeneo yenye umeme kuendelea kulipia Sh.27,000 ili maeneo hayo nayo yatumie umeme huo uliopo katika maeneo hayo. Ahsante.