Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 87 2019-09-11

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka Walimu wa Sayansi katika Mkoa wa Katavi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2016/2017 hadi 2018/2019, Serikali imeajiri jumla ya watumishi 7,515 katika shule za sekondari nchini. Kati yao, Walimu 7,218 na Fundi Sanifu Maabara 297. Kati ya walimu walioajiriwa walimu wenye mahitaji maalum walikuwa 29, walimu wenye elimu maalum ni 50 na walimu wa masomo ya sayansi na hisabati ni 7,089 na walimu wa lugha (Literature in English) walikuwa 100.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha mwaka 2016/2017 hadi 2018/2019 Serikali ilipanga jumla ya Watumishi 121 katika shule za sekondari Mkoani Katavi. Kati yaoWalimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati walikuwa 115 na Fundi Sanifu Maabara walikuwa Sita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuajiri watumishi wa kada mbalimbali ikiwemo walimu kwa kadri ya upatikanaji wa fedha. Ahsante. (Makofi)