Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 86 2019-09-11

Name

Rashid Mohamed Chuachua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Primary Question

MHE. DKT. RASHID M. CHUACHUA aliuliza:-

Jimbo la Masasi lina Shule moja tu ya Sekondari ya Kidato cha Tano na Kidato cha Sita ambayo ni ya Kitaifa ingawa mahitaji ya Wanafunzi wanaofaulu kwenda Kidato cha Tano na Kidato cha Sita yameongezeka sana, Shule pekee ya Kidato cha Tano na Kidato cha Sita iliyopo Masasi ni Shule ya Sekondari ya Wasichana Masasi:-

(a) Je, ni lini Serikali itazipandisha hadhi Shule za Sekondari za Mwenge Mtapika na Anna Abdallah ili ziweze kupokea Wanafunzi wa Kidato cha 5 na 6;

(b) Jimbo la Masasi linahitaji vyumba 27 vya maabara ambapo hadi sasa vyumba Saba tu ndiyo vina vifaa vya maabara katika shule Nne; Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa vya maabara katika Shule zote za Sekondari?

(c) Ikama ya Walimu wa Sayansi katika shule za Sekondari Tisa zilizopo Jimbo la Masasi ni Walimu 84 japokuwa waliopo ni 24 tu; Je, Serikali inaweza kulifanya jambo hili kama dharura inayohitaji utatuzi wa haraka kwa kutuletea Walimu 60 wa Sayansi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Rashid Mohamed Chuachua, Mbunge wa Masasi Mjini, lenye sehemu (a), (b), na (c), kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Masasi Mji inafanya jitihada kuziwezesha shule tatu za Sekondari ambazo ni Sululu, Mtapika na Anna Abdallah ili ziweze kupandishwa hadhi na kuanza kutoa elimu ya Kidato cha Tano na cha Sita. Tayari shule hizo zilishakaguliwa na wadhibiti ubora wa shule na kukutwa na mapungufu kadhaa, hasa ya miundombinu ya maji, umeme na mabweni na hivyo kukosa sifa. Halmashauri kwa kushirikiana na wadau inafanyia kazi mapungufu hayo ili shule hizo ziweze kupandishwa hadhi na kutoa elimu tarajiwa.

(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2017/2018, jumla ya shule za sekondari 1,800 zilizokamilisha ujenzi wa maabara zilipelekewa vifaa vya maabara, na kati ya hizo shule sita ni za Halmashauri ya Mji wa Masasi. Vilevile katika Mwaka wa Fedha 2018/2019, jumla ya shule 1,258 zilizokamilisha ujenzi wa maabara zitapelekewa vifaa vya maabara na taratibu za manunuzi zinaendelea ambapo shule tatu kati ya shule zitakazopatiwa vifaa hivyo zipo katika Halmashauri ya Mji wa Masasi.

(c) Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017 hadi 2018/2019, Serikali imeajiri jumla ya watumishi 7,515 katika shule za sekondari nchini. Kati yaoWalimu ni 7,218 na Fundi Sanifu Maabara ni 297. Kati ya walimu walioajiriwa walimu wenye mahitaji maalum ni 29, walimu wenye elimu maalum ni 50, walimu wa masomo ya sayansi na hisabati ni 7,089 na walimu wa lugha (Literature in English) ni 100. Ambapo walimu 15 wa sayansi walipangwa katika Halmashauri ya Mji wa Masasi. Ahsante.