Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 5 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 62 2019-09-09

Name

Issa Ali Abbas Mangungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ISSA A. MANGUNGU aliuliza:-

Tangu TRA ianze kukusanya kodi ya majengo imekusanya kiasi gani katika Mkoa wa Kodi Temeke kwa mwaka 2017/2018 na ni asilimia ngapi ya lengo?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ali Mangungu, Mbunge wa Mbagala, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Mapato Tanzania ilianza kukusanya kodi ya majengo (property rate) katika Mwaka wa Fedha 2016/2017 baada ya marekebisho ya Sheria ya Fedha ya Mamlaka za Serikali za Mitaa Sura 290 kufanyika kupitia Sheria ya Fedha ya mwaka 2016. Katika Mwaka wa Fedha 2017/2018, Mkoa wa Kikodi wa Temeke ulikusanya jumla ya shilingi 3,707,731,450 ikiwa ni sawa na asilimia 60 ya lengo la kukusanya jumla ya shilingi 6,197,367,187.