Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 56 2019-09-09

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA (K.n.y. MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA) aliuliza:-

Waendesha pikipiki (bodaboda) nchini wamekuwa wakikamatwa na Askari wa Usalama Barabarani mara kwa mara kwa tuhuma za makosa mbalimbali:-

Je, zoezi hili la ukamataji wa waendesha pikipiki limefanikiwa kwa kiasi gani?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Emanuel Mwakasaka, Mbunge wa Tabora kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, moja ya chanzo cha ajali za barabarani huchangiwa na waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda. Mathalan mwaka 2016 nchini kote kulitokea jumla ya ajali za pikipiki 2,544 zilizosababisha vifo vya watu 890 na majeruhi 2,128. Mwaka 2017 zilitokea ajali za pikipiki 1,459 zilizosababisha vifo vya watu 728 na majeruhi 1,090. Mwaka 2018 zilitokea ajali za pikipiki 876 ambazo zilisababisha vifo vya watu 366 na majeruhi 694.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Januari hadi Juni, 2019 kumetokea ajali za pikipiki 334 zilizosababisha vifo 176 na majeruhi 289. Ukilinganisha na kipindi kama hicho cha Januari hadi Juni, 2018 ambapo ajali zilitokea 408 zikasababisha vifo 165 na majeruhi 344, utaona kuwa ajali za pikipiki zimepungua sawa na asilimia 18 ingawa vifo viliongezeka kwa idadi ya 11 ambayo ni sawa na asilimia 6.6 na majeruhi kupungua kwa idadi ya 55 ambayo ni sawa na asilimia 16. Kwa ujumla takwimu hizi zinathibitsha kupungua kwa ajali za bodaboda barabarani ambazo zinatokana na waendesha pikipiki kutozingatia sheria.

Mheshimiwa Spika, kupungua kwa ajilia hizi ni mafanikio yanayopatikana kutokana na usimamizi wa Sheria za Usalama Barabarani kwa kuwachukulia hatua waendesha bodaboda ambao wanakiuka sheria na kuwachukulia hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwafikisha Mahakamani.