Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 55 2019-09-09

Name

Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL aliuliza:-

Halmashauri ya Manispaa ya Moshi kwa muda mrefu imekuwa na maombi ya kupandishwa hadhi kwa Zahanati za Msarango, Longuo B na Shirimatunda kuwa Vituo vya Afya:-

Je, ni lini Zahanati hizo zitapandishwa hadhi kuwa Vituo vya Afya?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Raphael Japhary Michael, Mbunge wa Moshi Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Manispaa ya Moshi ina jumla ya Zahanati 31, 12 za Serikali, tatu za Mashirika ya Dini na 16 binafsi. Vituo vya Afya viko 10. Viwili vya Serikali, kimoja cha Shirika la Dini na saba ni vya watu binafsi; na Hospitali nne zote za Mashirika ya Dini ambapo Serikali imeingia mkataba na Hospitali ya St. Joseph kuwa hospitali teule kwa maana ya CDH.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Mwongozo wa Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMAM) Kituo cha Afya kinapaswa kuhudumia wakazi kati ya 10,000 hadi 60,000. Zahanati inapaswa kuhudumia wakazi wasiozidi 10,000 na hospitali ina wakazi kuanzia 50,000 na kuendelea. Zahanati ya Msarango inahudumia wakazi 7,699, Longuo B wakazi 6,632 na Shirimatunda wakazi 4,485, hivyo, zinakosa sifa ya kupandishwa hadhi kuwa vituo vya afya.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI inasisitiza kujenga Vituo vya Afya vipya badala ya kuhuisha Zanahati izopo ili kuendana na ubora wa miundombinu inayohitajika na pia kuongeza idadi ya vituo vya kutolea huduma za afya na siyo kupunguza zahanati zilizopo ili kuongeza Vituo vya Afya.