Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 68 2019-11-11

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLA JUMA aliuliza:-

Je, Serikali ina mfumo gani wa kupandishwa daraja askari wenye vyeo vya chini?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika,kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Asha Abdulla Juma, Mbunge wa Viti Maalumkama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika,Vyombo vya Usalama vilivyo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi vina mfumo wa Upandishwaji wa madaraja kwa askari wa vyeo vya chini ambayo huzingatia vigezo mbalimbali ikiwemo umbele kwa maana ya seniority, miaka mitatu ya cheo alichonacho, tabia njema, nidhamu, utendaji mzuri, umahiri wa kazi, elimu au utaalamu mahsusi, uwezo wa kumudu madaraka ya cheo anachopandishwa, kutokuwa na tuhuma zinazochunguzwa wala mashtaka ya Kijeshi katika kipindi cha miaka mitatu na bajeti tengefu kwa mwaka husika.