Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 58 2019-11-11

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza:-

Kuna upungufu mkubwa wa Walimu katika Shule za Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba:-

Je, ni lini Serikali itapeleka walimu wa kutosha katika Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la mama yangu Mheshimiwa Conchesta Leonce Rwamlaza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba ina jumla ya shule za msingi za Serikali 141 zenye jumla ya wanafunzi 80,224. Halmashauri ina walimu 1,172 wa shule za msingi kati ya walimu 1,783 wanaohitajika hivyo kuwa na upungufu wa walimu 611.

Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kutatua changamoto ya upungufu wa walimu nchini kuanzia Mei, 2017 hadi Oktoba 2019, Serikali imeajiri walimu 15,480 wa shule za msingi, walimu 7,218 wa shule za sekondari na fundi sanifu wa maabara 297 ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba imepatiwa walimu 66 wa shule za msingi yaani 37 ajira mpya na 29 walihamishiwa kutoka sekondari kwenda shule za msingi. Serikali itaendelea kuajiri walimu wa shule za msingi na sekondari kwa kadri fedha na vibali vitakavyopatikana?