Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 55 2019-11-08

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. NAGU aliuliza:-

Je, ni lini miradi ya visima vya Waranga, Dumbeta, Endamudagya, Gidika, Murumba na Hirbadaw itakamilika na kuanza kusambaza maji kwa wananchi?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mary Michael Nagu Mbunge wa Hanang kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutatua changamoto ya maji katika vijiji vya Waranga, Dumbeta, Endamudagya, Gidika, Murumba na Hirbadaw, Serikali katika mwaka wa fedha 2017/2018 ilichimba visima vitano (5) vyenye uwezo wa kuzalisha maji kiasi cha mita za ujazo 45 kwa saa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuhakikisha visima hivyo vinatoa huduma ya maji kwa wananchi, katika mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali kupitia Programu ya Usambazaji Maji Endelevu Vijjini na Usafi wa Mazingira imetenga Kiasi cha Shilingi milioni 800 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya usambazaji maji katika vijiji vya Dumbeta, Waraga na Hirbadaw. Aidha, jumla ya vituo 30 vya kuchotea maji vitajengwa katika vijiji hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa miundombinu ya kusambaza maji katika visima vingine vilivyobakia vya Gidika, Endamudagya na Murumba utafanyika katika mwaka ujao wa fedha 2020/2021.