Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Madini 54 2019-11-08

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa utekelezaji mipango yake pamoja na maelekezo ya Mhe. Rais ya kushughulikia kero za wachimbaji wadogo hususani katika maeneo ya uchimbaji ya Ng’apa Mtoni na Muhuwesi?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Napenda kujibu swali la Mheshimwa Engineer Ramo Matala Makani (Mbunge wa Tunduru Kaskazini) kama ifuatavyo;-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Madini ya mwaka 2010 na marekebisho yake ya mwaka 2017 inatambua umuhimu wa wachimbaji wadogo. Wizara kupitia Tume ya Madini inatoa leseni za uchimbaji mdogo ambazo ni maalum kwa watanzania pekee. Aidha, Juhudi hizo ni pamoja na kuwapatia na kuwatengea maeneo mbalimbali ya kuchimba na kuanzisha masoko ya madini katika mji wa Tunduru ambapo Soko la Madini lilifunguliwa tarehe 27 Mei, 2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuwasaidia wachimbaji wadogo Mkoa wa Ruvuma na Wilaya ya Tunduru mwaka 2012/2013 Serikali ilitenga eneo la Mbesa lenye ukubwa wa hekta 15,605.30 kwa GN Na. 25 la tarehe 22 Februari, 2013 kwa ajili ya uchimbaji wa madini ya shaba na jumla ya leseni ndogo 441 zilitolewa kwa wachimbaji wadogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya leseni kubwa za utafiti ambazo zilikuwa hazifanyiwi kazi kufutwa, Wizara ya madini kupitia Tume ya Madini imetenga eneo la Ng’apa Mtoni kwa ajili ya shughuli za wachimbaji wadogo wa madini ya vito lenye ukubwa wa hekta 7,548.59.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Katika eneo la mto Muhuwesi uchimbaji unafanyika kwa kuzingatia masharti ya Sheria ya Madini za Mwaka 2010 na marekebisho yake ya mwaka 2017 na Sheria ya Mazingira ya Mwaka 2004. Aidha, kila mmiliki wa leseni ya uchimbaji ndani ya Mto Muhuwesi anatakiwa kupata vibali kutoka mamlaka husika (NEMC na Bonde la Ruvuma na Pwani ya Kusini) kabla ya kuanza kufanya shughuli za uchimbaji madini ndani ya Mto.