Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 31 2019-11-07

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM aliuliza:-

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji unatarajiwa kufanyika mwezi Novemba, 2019:-

Je, Serikali inasema nini juu ya ushirikishwaji wa Vyama vya Siasa katika mkakati wa kutoa elimu ili kufikia lengo la uchaguzi huru na haki?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Masoud Abdallah Salim, Mbunge wa Mtambile, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi wa Viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa ngazi ya Vijiji, Vitongoji na Mitaa za mwaka 2019, chini ya Matangazo ya Serikali ya Na. 371, 372, 373 na 374 ya mwaka 2019, Ofisi ya Rais, TAMISEMI imeandaa Mwongozo wa Elimu ya Mpiga Kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mwaka 2019. Mwongozo huo umevitambua Vyama vya Siasa kama mdau muhimu katika suala la utoaji wa Elimu ya Mpiga Kura.

Aidha, katika hatua za maandalizi ya Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019, wadau wote muhimu vikiwemo Vyama vya Siasa vyenye usajili wa kudumu vilishirikishwa katika hatua zote na kutoa maoni yao ili kuwezesha kuwa na Uchaguzi Huru na Haki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni imani yetu kuwa Vyama vyote vya Siasa vitashiriki katika kutoa elimu ya mpiga kura kwa wanachama wao kwa kuzingatia miongozo na Kanuni zilizotolewa.