Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 22 2019-11-06

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO (K.n.y. MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU) aliuliza:-

Mkoa wa Kagera una vijiji 134 ambavyo havijafikiwa na umeme wa REA; Biharamulo Vijiji 29, Bukoba Vijiji 9, Karagwe Vijiiji 8, Kyerwa Vijiji 31, Misenyi Vijiji 5, Muleba Vijiji 25 na Ngara Vijiji 27:-

(a) Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA katika Vijiji hivyo?

(b) Umeme wa REA ulifika kwenye vijiji vingi lakini haukusambazwa: Je, mradi wa ujazilizi utaanza lini Mkoani Kagera ili wananchi waliorukwa wapatiwe umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bernadetha Kasabago Mushashu lililoulizwa na Mheshimiwa Halima Bulembo, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi kabambe wa kupeleka umeme katika vijiji vyote nchini kufikia mwezi Desemba, 2021. Kwa sasa Mkandarasi Nakuroi anaendelea na kazi ambapo kufikia mwezi Oktoba, 2019 vijiji 82 vimewashwa umeme katika Mkoa wa Kagera na kazi ya uunganishaji wa wateja inaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vyote vitakavyosalia katika Mkoa wa Kagera vitapatiwa umeme kupitia mradi wa REA awamu ya pili, unaozunguka kuanza sasa ambao utakamilika mwezi Januari, 2020. Pia kukamilika kwa mradi huu mwezi Desemba, 2021 kutapeleka umeme katika maeneo yote katika Mkoa wa Kagera pamoja na Vitongoji vyake.

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa ujazilizi awamu ya pili (Densification IIA) utatekelezwa katika Mikoa tisa na utaanza kutekelezwa kuanzia mwezi Novemba, 2019 hadi mwezi Juni, 2020. Mradi wa ujazilizi katika Mkoa wa Kagera utaanza kutekelezwa kupitia mradi wa ujazilizi awamu ya IIB (Densification IIB) utakaoanza kutekelezwa kuanzia mwezi Julai, 2020 na kukamilika mwezi Machi, 2021. (Makofi)