Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 21 2019-11-06

Name

Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA BAKARI MBAROUK aliuliza:-

Tanzania ina jumla ya Majiji sita likiwemo Jiji la Tanga; katika Majiji hayo kuna maeneo ambayo yako nje ya Jiji ambayo ni Mitaa, Vitongoji na Vijiji (Perry Urban); Kitengo cha Perry Urban kimekabidhiwa jukumu la kusambaza umeme wa REA III katika Majiji:-

Je, ni lini Perry Urban itaanza kusambaza umeme katika Jiji la Tanga?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mussa Bakari Mbarouk, Mbunge wa Tanga Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea na utekelezaji wa miradi ya umeme iliyopo katika vijiji, vitongoji na maeneo mbalimbali kandokando ya miji na vijiji yaani Perry Urban. Awamu ya kwanza ya utelelezaji wa mradi huu umeanza katika Mkoa wa Dar es Salaam na Mkoa Pwani na kwa upande wa Dar es Salaam katika Wilaya ya Kigamboni. Utekelezaji wa mradi huu utakamilika mwezi Aprili, 2020. Baada ya kukamilika kwa mradi huu, Serikali itaanza kutekeleza mradi huu katika Mikoa yote nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jiji la Tanga Serikali imekamilisha upembuzi yakinifu na kubainisha kuwa miradi wa kupeleka umeme maeneo ambayo yako kandokando ya Jiji la Tanga unahusisha ujenzi wa njia ya msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 15, ufungaji wa transfoma 15 kati ya hizo transfoma 4 ni za KVA 200, transfoma sita za KVA 100 na 5 za KVA 50.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi ya Perry Urban katika Jiji la Tanga pia utahusisha ujenzi wa njia ya Msongo wa kilovoti 11 yenye urefu wa kilomita 48.8, ufungaji transfoma 35; na kati ya hizo transfoma nane ni za 200KVA, 20 za 100KVA na saba za KVA 50. Kazi nyingine ni kuvuta laini ndogo ya kV 0.4 yenye urefu wa Kilomita 200. Wateja wa awali watakaonufaika na mradi huu katika Jiji la Tanga ni 5,125 ambao wanatarajiwa kupata umeme katika maeneo hayo. Utekelezaji wa mradi huu utaanza mwezi Julai, 2020 na kukamilika mwezi Machi, 2021. Gharama za mradi huo ni shilingi bilioni 7.5.