Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 18 2019-11-06

Name

Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KABWE Z. R. ZITTO aliuliza:-

Katika kutekeleza mpango wa kutuma fedha za elimu moja kwa moja mashuleni Serikali hutuma shilingi bilioni 18 kila mwezi kwenye akaunti za shule nchini kwa mujibu wa maelezo ya viongozi kwa umma?

(a) Je, Serikali imeshatuma kiasi gani cha fedha kati ya Januari – Desemba, 2016, 2017 na 2018 kwenda kwenye shule nchini?

(b) Je, Serikali imefanya ukaguzi wa matumizi ya fedha hizo na kama zilizotoka Hazina zilifika kwenye shule husika; Je, Serikali ipo tayari kuleta Bungeni Ripoti za Ukaguzi huo?

(c) Kama Serikali haijafanya ukaguzi huo; Je, ipo tayari kuagiza ukaguzi maalum utakaofanywa na CAG na kuweka Taarifa ya Ukaguzi huo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kabwe Ruyagwa Zitto, Mbunge wa Kigoma Mjini, lenye sehemu (a), (b) na (c), kwa pamoja kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutekeleza Mpango wa Elimu msingi Bila Malipo kuanzia Januari, 2016 hadi Disemba, 2018 jumla ya Sh.798,170,400,005.04 zimetolewa na Serikali na kutumwa moja kwa moja shuleni. Fedha hizo zimejumuisha chakula kwa wanafunzi, fidia ya ada, uendeshaji wa shule, posho ya madaraka kwa Wakuu wa Shule na Walimu Wakuu na Maafisa Elimu wa Kata. Fedha hizi zinajumuisha pia fedha zinazokwenda Baraza la Mitihani kwa ajili ya maandalizi ya mitihani ya Kitaifa kwa ngazi husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika utaratibu wa kawaida wa ukaguzi wa fedha za Serikali, Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali hufanya ukaguzi katika Wizara, Taasisi, Mashirika ya Umma na Mamlaka za Serikali za Mitaa kila mwaka. Kwa kuwa, fedha za Elimu Msingi Bila Malipo ni sehemu ya fedha zinazotumwa katika Mamlaka za Serikali za Mitaa na kwa kuwa fedha hizo hutengwa kwenye bajeti kila mwaka wa fedha, ni dhahiri kuwa fedha hizo hukaguliwa na CAG pale anapofanya ukaguzi kwenye mamlaka husika. Ahsante.