Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 1 Water and Irrigation Wizara ya Maji 9 2019-11-05

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:-

Mradi wa maji katika Kata ya Mtwango bado haujakamilika:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi huo ambao umechukua muda mrefu bila kukamilika?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwa ruhusa yako kwanza naomba nitoe pole kwa wananchi wa Jimbo langu la Pangani pamoja na wananchi wa Mkoa wa Tanga kwa mafuriko ambayo yalikuwa yametokea, tumepoteza ndugu zetu lakini pia kuharibika kwa miundombinu. Tunamshukuru Mkuu wa Mkoa kwa hatua ya haraka ya kuweza kurejesha miundombinu ile.

Mheshimiwa Spika, sasa kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mendrad Lutengano Kigola, Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli Mradi wa Maji wa Kata ya Mtwango umechukua muda mrefu kutokana na changamoto iliyokuwepo ya wakandarasi kutokamilisha kazi kwa wakati hali ambayo ililazimu kuwaondoa.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2019/ 2020, Serikali imetenga shilingi milioni 300 kwa lengo la kukamilisha mradi huo. Kazi zitakazofanyika ni ujenzi wa matenki, ununuzi wa pampu na ununuzi wa mabomba ya kusambaza maji kwa wananchi. Kazi hizo zitafanywa na wataalam na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini yaani RUWASA katika ngazi ya wilaya na mkoa. Taratibu za kukamilisha kazi zilizobaki katika Kijiji cha Sawala zinaendelea. Mradi huo unategemewa kukamilika katika mwaka wa fedha 2019/2020.