Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 29 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 247 0000-00-00

Name

Tauhida Cassian Gallos Nyimbo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR (K.n.y MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOSS NYIMBO) aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka uzio kwenye vituo vikubwa vya Polisi vilivyopo Zanzibar?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tauhida Cassian Galloss, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inao mpango wa kujenga uzio katika Vituo na Makambi yote ya Polisi Tanzania. Aidha, Jeshi la Polisi kwa kutumia rasilimali zilizopo eneo husika, limekuwa likijenga uzio wa muda au wa kudumu katika maeneo mbalimbali na litaendelea kujenga uzio katika vituo zaidi hatua kwa hatua.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Zanzibar, Serikali imeanza kujenga uzio kwa baadhi ya maeneo ya Kambi ya Ziwani Zanzibar, mathalani eneo la Chuo Ujenzi umeanza kwa kutumia fedha zilizotokana na mapato ya ndani. Aidha, kwa upande wa mbele ujenzi unafanyika sambamba na kujenga maduka ambayo yatasaidia kuendesha shughuli za Polisi na kujiingizia mapato.