Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 9 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 113 2020-02-07

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE (K.n.y. MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) aliuliza:-

Utalii wa uwindaji, utalii wa picha na ufugaji wa mapori ya misitu na Hifadhi ya Ugunda, Isuvangala na Ipembampazi ni miongoni mwa fursa kuu za utalii kwenye Jimbo la Sikonge:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Uwanja wa Ndege uliokuwa umeanza kujengwa karibu na Mlima wa Ipole ambao ulijumuisha pia ujenzi wa nyumba za kufikia watalii (tourist rest houses) kwenye Kijiji cha Ugunda?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph George Kakunda, Mbunge wa Jimbo la Sikonge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imeendelea kuimarisha miundombinu katika maeneo mbalimbali ya hifadhi nchini ili yaweze kufikika kwa urahisi na muda wote wa mwaka. Lengo kuu ni kuwezesha watalii kuyafikia maeneo hayo na hivyo kuiongezea mapato Serikali. Aidha, katika kuimarisha ulinzi wa rasilimali za wanyamapori katika Pori la Akiba Ugalla, mwaka 2005, Wizara ilifanya maandalizi ya ujenzi wa uwanja mdogo wa ndege (airstrip) karibu na Milima ya Ipole. Kazi ya awali iliyofanyika ikiwa ni maandalizi ya kutengeneza uwanja husika ilikuwa ni kuweka mipaka kwa kufyeka miti.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2006, Wizara ya Maliasili na Utalii iliomba Mamlaka ya Viwanja vya Ndege ifanye tathmini ya eneo hilo ili kuona kama linakidhi vigezo vinavyotakiwa kwa mujibu wa sheria. Mamlaka ya Viwanja vya Ndege ilibaini kuwa eneo pendekezwa lipo katikati ya milima na hivyo kupelekea usalama kuwa mdogo kwa ndege kutua na kuruka. Kutokana na ushauri huo, Wizara ya Maliasili ilisitisha maandalizi ya ujenzi wa uwanja husika na kujikita zaidi kuimarisha viwanja vilivyopo ndani ya Pori la Akiba Ugalla.