Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 106 2020-02-07

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA (K.n.y. MHE. MARGARET S. SITTA) aliuliza:-

(a) Je, Serikali ipo tayari kuangalia bajeti ya Hospitali ya Wilaya ya Urambo ambayo inahudumia wananchi wa maeneo ya Kaliua, Ulyankulu na maeneo ya jirani ili kuongeza uwezo wa kutoa huduma?

(b) Hospitali ya Wilaya ya Urambo ina majengo mawili ya ICU na maabara ambayo hayajakamilika tangu yalipoanza kujengwa 2011 kupitia utaratibu wa LGDG ya mradi wa ADB. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu ombi la wananchi wa Urambo la shilingi milioni 200 ambazo zinaweza kumaliza majengo hayo?

(c) e, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kuongeza wafanyakazi angalau Manesi 12 na Wafamasia 6 kutokana na kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa Hospitalini hapo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Urambo lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Naibu Spika, ili kupunguza msongamano wa wagonjwa kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Urambo, Serikali imepanua Kituo cha Afya Ulyankulu, Kituo cha Afya Usoke na kujenga Kituo cha Afya Usoke Mlimani kwa gharama ya jumla ya shilingi bilioni 1.2. Mpango huu utasaidia kuimarisha utoaji wa huduma za afya katika vituo hivyo na kupunguza idadi ya wagonjwa wanaokwenda kutibiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Urambo.

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli mradi wa ujenzi wa majengo ya upasuaji, ICU na maabara uliofadhiliwa na ADB haukukamilika kutokana na tatizo la kukisia chini ya kiwango gharama za ujenzi wa majengo hayo. Serikali imepanga kukamilisha ujenzi wa majengo hayo kwa kutenga fedha kupitia bajeti ya mwaka wa fedha 2020/2021.

(c) Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa Fedha 2018/2019, jumla ya watumishi wapya 26 wa kada ya Wauguzi, Madaktari, Maafisa Tabibu, Mtaalam wa Mionzi na Maabara walipangwa kufanya kazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Urambo. Serikali itaendelea kuajiri na kuwapanga watumishi wa kada za afya kadri watakavyokuwa wakipatikana.