Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 102 2020-02-06

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. KHATIB SAID HAJI aliuliza:-

Ni kosa la Jinai kwa Mtu au Vyombo vya Habari kutoa, kuandika, kusambaza au kutangaza habari za uongo. Je, Jeshi la Polisi linachukua hatua gani stahiki kwa watu au vyombo vya habari vinavyofanya makosa hayo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI YA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Khatibu Said Haji, Mbunge wa Konde, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi linao utaratibu unaotumika pindi mtu anapokuwa ametenda makosa ya jinai ambapo ushahidi hukusanywa kisha jalada huandaliwa kwenda kwa Mwanasheria wa Serikali; na ushahidi ukijitosheleza, mtuhumiwa hufikishwa Mahakamani.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina mamlaka kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari Na. 12 ya Mwaka 2016 ambapo inaelekeza kuchukua hatua kwa chombo cha habari kilichotoa taarifa za uongo ikiwa ni pamoja na kufuta leseni au kusimamisha leseni kwa muda pale ambapo chombo cha habari kimekiuka masharti ya leseni hiyo.