Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 8 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 101 2020-02-06

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA aliuliza:-

Umeme umekuwa ukikatika mara kwa mara Korogwe na kufanya uharibifu wa mali za Wananchi:-

Je, ni lini tatizo hilo litapatiwa ufumbuzi.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mary Pius Chatanda, Mbunge wa Korogwe Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kutokana na ukarabati wa miundombinu ya umeme unaoendelea kwa sasa Wilayani Korogwe, TANESCO hulazimika kukata umeme katika maeneo husika ya wilayani humo ikiwa ni pamoja na maeneo ya Mji wa Korogwe. Hali hiyo inasababishwa na kazi zinazoendelea za kukarabati wa miundombinu ikiwa ni pamoja na kubadilisha vikombe vibovu, nguzo mbovu, ukataji wa miti na matawi katika njia za umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kazi za kukarabati miundombinu ya kusambaza umeme zifanyike hulazimika kuzima umeme katika maeneo yanayofanyiwa ukarabati. Kukamilika kwa ukarabati unaoendelea kutawezesha kuimarika kwa umeme na kurudi katika hali yake ya kawaida.

Mheshimiwa Naibu Spika, mara zote kabla ya kuzima umeme taarifa zimekuwa zikitolewa katika vyombo mbalimbali vya habari katika Wilaya ya Korogwe na Mkoa wa Tanga. Hali ya kukatika umeme kwa ajili ya kupisha matengenezo kumeimarisha sana upatikanaji wa umeme katika maeneo hayo. Aidha, tunaomba wananchi waendelee kuwa wavumilivu katika kipindi cha matengenezo ya miundombinu hiyo.