Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 51 2019-09-06

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. NAGHENJWA L. KABOYOKA) aliuliza:-

Umeme wa maji unaonekana kuwa wa bei nafuu, na Same kuna maporomoko ya Mto Hingilili yanayoangukia Kata ya Maore na ya Mto Yongoma yanayoangukia Kata ya Ndungu; na Chuo cha Ufundi Arusha wameonesha utaalamu mkubwa wa kutengeneza umeme kwa kutumia maji hayo:-

Je, Serikali ipo tayari kukiwezesha Chuo hicho ili kiweze kujenga mitambo ya kuzalisha umeme wa maji Kata za Maore na Ndungu?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge wa Same Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua muhimu ya awali katika uendelezaji wa mradi wa kufua umeme ukiwemo wa maporomoko ya maji ni kufanya upembuzi yakinifu ambapo pamoja na mambo mengine tathmini ya wingi wa maji katika kipindi cha kuzalisha umeme (water resource assessment) lengo ni kujua kiasi cha umeme utakaozalishwa na gharama za kutekeleza mradi na manufaa yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali kupitia TANESCO na wadau wengine inaendelea kufanya tathmini za awali katika vyanzo mbalimbali vya kuzalisha umeme wa maporomoko ya maji makubwa na madogo ikiwemo maporomoko ya Mto Hingilili. Tathmini hizo zitafanyiwa kazi kulingana na matokeo yake na maeneo yanayohusika yatajulishwa ikiwa ni pamoja na Chuo cha Ufundi Arusha.