Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 42 2019-09-06

Name

Justin Joseph Monko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO aliuliza:-

Katika mitihani ya Taifa ya Vitendo kwa Kidato cha Nne utaratibu mpya ulioanzishwa mwaka 2017 ambao ni bora zaidi ulibadilika na kupelekewa checklist ambayo sasa inahitaji vifaa vingi zaidi na practical nyingi ikilinganishwa na hapo awali ambapo ‘instructions’ ya mwezi mmoja ilitolewa kabla:-

(a) Je, Serikali iko tayari kuongeza fedha za vifaa vya Maabara kufidia ongezeko la gharama za vifaa hivyo ambavyo vinazidi fedha iliyoingizwa kwa mwaka?

(b) Shule nyingi sasa zimelundika madeni ya Maabara na hushindwa kulipa: Je, Serikali iko tayari kulipa madeni haya yaliyosababishwa na utaratibu huu mpya?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Justin Joseph Monko, Mbunge wa Singida Kaskazini, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ilitekeleza Sera ya Elimu Msngi bila malipo tangu mwaka 2016 ambapo kila mwezi takribani shilingi bilioni 23.8 zimekuwa zikitumwa moja kwa moja shuleni. Kati ya fedha hizi, takribani shilingi bilioni 1.645 zinatolewa kwa ajili ya ruzuku ya uendeshaji wa shule (Capitation Grand). Matumizi ya fedha za ruzuku ya uendeshaji ni pamoja na kununua vifaa vya kufundishia na kujifunzia, ikiwa ni pamoja na vifaa vya maabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia programu ya EP4R, Serikali imekuwa ikinunua vifaa vya maabara kwa shule mbalimbali za sekondari nchini. Mwaka wa fedha 2017/2018, jumla ya shule 1,800 za sekondari zilizokuwa zimekamilisha ujenzi wa maabara zao, hazikuwa na vifaa, vilipelekewa vifaa hivyo. Aidha, mwaka 2018/2019, jumla ya shule 1,258 zilizokamilisha maabara, zimeainishwa na ununuzi wa vifaa hivyo upo kwenye hatua za mwisho. Pindi taratibu zitakapokamilika, shule hizo zitasambaziwa vifaa hivyo vya maabara, ambapo katika Mkoa wa Singida kuna shule 59 zitakazopatiwa vifaa vya maabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilianza kutekeleza utaratibu wa kupelekea fedha moja kwa moja shuleni mwaka 2016 na hivyo madeni mengi yanayozungumziwa ni ya kabla ya mwaka 2016, ambapo shule zilikuwa zikikusanya ada na kuruhusiwa kutumia kwa ajili ya uendeshaji wa shule ikiwemo ununuzi wa vifaa vya maabara. Hivyo Serikali imeelekeza Mamlaka za Serikali za Mitaa kulipa madeni hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.