Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 3 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 33 2019-09-05

Name

Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR aliuliza:-

Je, ni sababu gani zimekwamisha uanzishwaji wa Benki ya Wanawake kwa upande wa Zanzibar?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Faida Mohammed Bakar, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba kwa sasa hatuna Benki inayoitwa ya Benki Wanawake Tanzania, baada ya iliyokuwa Benki ya Wanawake Tanzania kuunganishwa na Benki ya TPB. Hivyo basi, huduma za iliyokuwa Benki ya Wanawake Tanzania zinaendelea kutolewa na Benki ya TPB ambapo Benki ya TPB imeanzisha dirisha maalum la akina mama katika matawi yake yote 76 yaliyopo nchini Tanzania, yakiwemo matawi ya Unguja na Pemba ili kukidhi mahitaji ya huduma za kibenki kwa akina mama kote nchini. Kwa muktadha huu, wanawake na wananchi wote wa Zanzibar wataendelea kuhudumiwa kupitia dirisha hilo maalum.