Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 17 2019-09-04

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:-

Kufuatia majibu ya Swali langu Na. 17 lililojibiwa tarehe 07/11/2018 kuhusu Bagamoyo kupata hadhi ya Halmashauri ya Mji, Serikali ilielekeza kwamba tusubiri wasilisho la Kamati ya ushauri ya Mkoa wa Pwani (RCC) ili Ofisi ya Rais (TAMISEMI) iweze kulifanyia kazi ombi hilo; na suala hilo limeshajadiliwa na RCC na taarifa kuwasilishwa Ofisi ya Rais (TAMISEMI):-

Je, ni lini sasa Serikali itaipa Bagamoyo hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA C. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa Mbunge wa Bagamoyo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mapendekezo ya kupandisha hadhi Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo kuwa Halmashauri ya Mji yaliwasilishwa kwenye barua yenye kumbu Na. CAB.51/222/01/56 ya terehe 23 Januari, 2019 kutokq kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani.

Mheshimiwa Naibu Spika, maombi hayo yalichambuliwa kulingana na mwongozo wa kuanzisha maeneo ya utawala wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo. Wilaya ya Bagamoyo ilikosa vigezo viwili muhimu ili kuiwezesha kupandishwa hadhi kuwa Halmashauri ya Mji. Vigezo vilivyokosekana ni kukosekana kwa mpango kabambe wa uendeshaji wa Mji (Master Plan) na eneo lake lililopimwa kuwa na chini ya asilimia 75. Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani amejulishwa kwa barua yenye kumbu Na. CCB.132/394/01B/30 ya tarehe 14 Machi, 2019.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Rais TAMISEMI itaendelea kutoa ushirikiano kwa uongozi na wananchi wa Mkoa wa Pwani wakati wote na jitihada zao ili kukamilisha vigezo ili kuiwezesha Bagamoyo kupandishwa hadhi kuwa Halmashauri ya Mji.