Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 77 2020-02-04

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:-

Jimbo la Tunduru Kusini lina changamoto ya maji kutokana na mabadiliko ya tabianchi:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuchimba visima virefu na vifupi katika kata ya Tuwemacho, Mchuluka, Mchoteka, Mbati, Marumba, Wenje, Nasomba, Namasakata na Lukumbule.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa maji naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate Mbunge wa Tunduru Kusini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi sasa Jimbo la Tunduru Kusini lina jumla ya miradi mitano ya maji ya bomba kwenye vijiji 11. Miradi hiyo ipo kwenye Kata za Mbati, Nalasi, Namasakata, Misechela, Mtina, Ligoma, Mchesi na Lukumbule. Aidha, Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo katika Sekta ya Maji Help for Underserved Communities imechimba visima 72 katika Kata za Tuwemacho, Marumba, Lukumbule Mbesa na Mtina. Visima hivyo vimefungwa pampu za mkono. Vilevile Wilaya ya Tunduru kwa kushirikiana na wadau wa Maendeleo ya Sekta ya Maji All Mother and Child Count imechimba visima virefu katika kata za Mchuluka, Namasakata, Chiwana na Lukumbule. Visima hivyo vitatumika kujenga miradi ya maji ya bomba katika maeneo hayo. Tayari utekelezaji umeanza kwa kata ya Chiwana na Namasakata

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha huduma ya maji inakuwa ya uhakika katika Wilaya ya Tunduru, Serikali kupitia Wakala ya Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini imetenga na kutoa fedha katika bajeti ya mwaka 2019/2020 kiasi cha shilingi milioni 974 kwa ajili ya kujenga, kukarabati na kufanya upanuzi wa miradi ya maji katika vijiji mbalimbali vilivyopo wilaya hiyo vikiwemo vijiji vya Jimbo la Tundurru Kusini. Vijiji hivyo ni Mbesa, Airport, Nasomba, Namasakata, Chiwana, Semeni, Nalasi, Misechela, Angalia, Ligoma na Mchekeni. Aidha, Serikali imepanga kuchimba visima Virefu viwili katika vijiji vya Wenje na Likweso vilivyopo Jimbo la Tunduru Kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga na kutoa fedha kadri zinavyopatikana ili kuweza kujenga na kukarabati miradi ya maji katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Jimbo la Tunduru Kusini ili wananchi waweze kunufaika na huduma ya majisafi na usafi wa mazingira.