Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 52 2020-02-03

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:-

Wananchi wa Wilaya ya Lushoto wamejitahidi kujenga maboma mengi ya maabara lakini mpaka sasa Serikali haijawaunga mkono:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuunga mkono juhudi hizo za wananchi kwa kumalizia maboma haya?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFlSI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shaabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Lushoto, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikisha nguvu za wananchi imekamilisha ujenzi wa vyumba vya maabara 13 katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto kati ya maabara 159 zinazohitajika.

Aidha, maabara 138 zinaendelea kujengwa kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri na nguvu za wananchi. Katika mwaka wa fedha 2019/20, Halmashauri inaendelea na hatua za mwisho za ukamilishaji wa maabara katika Shule za sekondari za Mlongwema, Kwemalamba, Lukozi, Ngwelo na Shume zilizopatiwa shilingi milioni 5 kupitia Programu ya Lipa Kulingana na Matokeo (EP4R).