Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2015-2020 | Session 18 | Sitting 4 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi | 50 | 2020-01-31 |
Name
Susan Anselm Jerome Lyimo
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SUSAN A. J. LYIMO aliuliza:-
Utaratibu wa marejesho ya Mikopo ya Elimu ya Juu umeendelea kukumbwa na changamoto kubwa hasa baada ya ongezeko la asilimia 6 kama retention fee na hivyo kusababisha wanufaika wa mikopo kushindwa kumaliza kurejesha mikopo hiyo?
Je, kwa nini Serikali isilete Muswada wa mabadiliko ya Sheria husika utakaokuwa na masharti rahisi kwa wanufaika ili waweze kumaliza kulipa mikopo kwa wakati?
Name
William Tate Olenasha
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ngorongoro
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-
Mheshimwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia napenda kujibu swali la Mheshimiwa Susan Anselm Lyimo Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu hutoza asilimia 6 kwenye salio la deni yaani outstanding loan balance la mnufaika kwa mkopo kama tozo ya kutunza thamani yaani value retention fee. Lengo la tozo hii ni kulinda thamani ya fedha wanazokopeshwa wanufaika wa mikopo ili kuwa na mfuko endelevu utakaoendelea kutoa mikopo kwa wahitaji wengine bila kulazimika kuongeza fedha zaidi kutokana na upotevu wa thamani ya fedha.
Mheshimiwa Spika, kumbukumbu zinaonyesha kuwa wanufaika wanaoanza kurejesha mkopo kwa wakati humaliza kati ya miaka 4 hadi 10 kulingana na kiwango cha mshahara. Hata hivyo, Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya urejeshaji wa mikopo kwa wanufaika ili kuwawezesha kurejesha na kumaliza madeni yao kwa wakati.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved