Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Madini 49 2020-01-31

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:-

Katika Jimbo la Nyang’hwale kuna maeneo mengi sana ya Wachimbaji wadogo wa madini ya Dhahabu kama vile Isakeli, Isonda, Lyulu, Nyamalapa, Lubando, Shibalanga na Kasubuya ambayo Wachimbaji hao wanafanya kazi na Dhahabu inapatikana bila utaratibu wowote?

(a) Je, ni lini Serikali itayarasimisha maeneo hayo na kuyagawa kwa Wachimbaji ili watambulike Kisheria na iwe rahisi kwa Serikali kukusanya kodi?

(b) Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake iliyoitoa mbele ya Waziri Mkuu ya kulitoa eneo la Bululu kwa Wachimbaji wadogo?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hussein Nassor Amar Mbunge wa Nyang‟wale lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Madini imedhamiria kuwaendeleza wachimbaji wadogo nchi nzima kwa kuwapatia maeneo ya uchimbaji ili waweze kuchangia uchumi kwa kulipa kodi, kujiajiri na kuongeza kipato cha Taifa.

Mheshimiwa Spika, Kampuni ya Nyanzaga Mining Co. Ltd iliyokuwa ikimiliki leseni ya utafiti Na. PL 9662 ya mwaka 2014 iliachia eneo lake lenye ukubwa wa eka 70 katika eneo la Bululu wilayani Nyang‟hwale. Aidha, eneo hilo limegawiwa kwa vikundi 22 vya uchimbaji wa madini ya dhahabu ambapo Tume ya Madini ilitoa leseni hizo tarehe 30 mwezi wa kumi na mbili mwaka 2019.

Mheshimiwa Spika, Eneo la Lubando lilikuwa na leseni ya uchimbaji wa kati wa Kampuni ya Busolwa Mining Co. Ltd. Hata hivyo, leseni hiyo ilifutwa na Serikali na kupewa wachimbaji wadogo. Aidha, eneo la Lyulu bado lina maombi ya leseni ya uchimbaji wa kati wa Kampuni ya Busolwa Mining Co. Ltd.

Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Tume ya Madini inaendelea na juhudi zake za kutafuta maeneo mengine kwa ajili ya wachimbaji wadogo ambapo Tume ya Madini imewataka wamiliki wote wa leseni kubwa za utafiti kutimiza matakwa ya sheria vinginevyo maeneo yao yatafutwa kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 na kupewa wachimbaji wadogo. Mwisho, Naomba kutoa wito kwa wamiliki wa leseni za utafiti wote nchini uchimbaji na wafanyabiashara wote wa madini kuendelea kuzingatia sheria za madini ikiwa ni pamoja na kuuza madini kwenye masoko yaliyofunguliwa nchini kote.