Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2015-2020 | Session 18 | Sitting 1 | Community Development, Gender and Children | Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto | 8 | 2020-01-28 |
Name
Sikudhani Yasini Chikambo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:-
Kumekuwa na wimbi kubwa la watoto wa mtaani ambao wanaishi katika mazingira magumu.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia watoto hao?
Name
Dr. Faustine Engelbert Ndugulile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kigamboni
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sikudhani Yassin Chikambo, Mbunge Viti Maalum kutoka Mkoa wa Ruvuma, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kumekuwa na wimbi kubwa la watoto wa mitaani ambao wanaishi katika mazingira magumu. Katika kipindi cha Januari hadi Disemba, 2019 jumla ya watoto 36,548 wakiwemo watoto wa kiume 17,894 na wa kike 18,654 walitambuliwa. Kati ya hao jumla ya watoto 1,178 walipatiwa huduma mbalimbali ikiwemo huduma za afya, msaada wa kisaikolojia na jamii, msaada wa kisheria, kuunganishwa na familia zao na kuwapatia elimu ya ujasiriamali.
Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mpango wa kuwaunganisha watoto na familia na kuwatafutia malezi mbadala wale wasio na familia katika Mkoa wa Mwanza. Programu hii imeanza kutekelezwa mwezi Novemba, 2019 na inatarajiwa kufika mikoa yote ambayo ina wimbi kubwa la watoto wanaoishi mitaani.
Mheshimiwa Spika, mwisho nichukue nafasi hii kuikumbusha jamii kuwa jukumu la matunzo, malezi, ulinzi na usalama wa mtoto ni la familia na jamii kwa ujumla. Vilevile Mamlaka ya Serikali za Mitaa zinapaswa kusimamia Sheria ya Mtoto Na. 21 ya mwaka 2009 ili kuwawajibisha wazazi wanaotelekeza majukumu yao na badala yake wanawaacha watoto kuzurura mitaani.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved