Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 4 2020-01-28

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:-

Kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu ya malimbikizo ya madeni mbalimbali ya wazabuni wanaotoa huduma mbalimbali ikiwepo huduma ya kupeleka chakula kwa wanafunzi magerezani na matengenezo ya magari.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kulipa madeni hayo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Emanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali katika nyakati tofauti imekuwa na mkakati wa kulipa madeni yake ya ndani ikiwemo madeni ya watoa huduma, chakula cha wafungwa na matengenezo ya magari katika magereza yote nchini.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2016/2017 hadi mwaka wa fedha 2018/2019 jumla ya kiasi cha fedha shilingi 23,563,630,710.61 zimelipwa kwa ajili ya watoa huduma za uendeshaji, chakula cha wafungwa na matengenezo ya magari yakiwa ni madeni ya mwaka wa fedha 2014/2015 hadi 2016/2017.

Mheshimiwa Spika, madeni ya mwaka 2012/2013 mpaka mwaka 2013/2014 na 2017/2018 tayari yameshahakikiwa, kinachosubiriwa ni fedha kutoka Hazina kwa ajili ya kulipa. Hata hivyo, madeni ya mwaka wa fedha 2018/2019 tayari yameandaliwa yanasubiri uhakiki kutoka Hazina ili kuhakiki madeni hayo na baadaye kuyalipa.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kulipa madeni ya wazabuni wanaotoa huduma mbalimbali ikiwemo chakula cha wafungwa na matengenezo ya magari kadri ya fedha itakavyopatikana.