Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 28 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 233 2019-05-15

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:-

Wananchi wanaoishi katika Jimbo la Kibiti hutumia nishati ya mkaa na kuni kwa matumizi ya nyumbani, shuleni, gerezani na kadhalika, hivyo kusababibisha uharibifu mkubwa wamazingira kwa kukata miti hovyo:-

(i) Je, Serikali ina mkakati gani wa kupeleka nishati mbadala?

(ii) Je, ni aina gani ya nishati itakayotumka badala ya kuni na mkaa?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swal la Mheshimiwa Ally Seif Ungado, Mbunge wa Kibiti, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Sera ya Taifa ya Nishati ya mwaka 2015 (The National Energy Policy, 2015) imetoa mwongozo wakuboresha maisha ya wananchi kwa matumizi bora ya nishati kupitia teknolojia ya kisasa badala ya kuni na mkaa. Aidha, Serikali imekuwa ikichukua jitihada za makusudi kuendeleza vyanzo mbalimbali vya nishati ili kuongeza mchango wa nishati mbadala katika upatikanaji wa nishati nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha muda wa kati kuanzia mwaka 2015 hadi 2020, Serikali inatekeleza miradi ya kuzalisha umeme kupitia vyanzo vya gharama nafuu vya maji na gesi ikiwa ni mkakati ya kuwawezesha wananchi kumudu kutumia nishati vya umeme wa gharama nafuu kwa ajili ya kupika badala ya kuni na mkaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeanza kutekeleza mradi wa kusambaza gesi asilia katika Miji ya Mtwara, LIndi, Pwani na Dar es Salaam ikiwa ni nishati mbadala ili kupunguza matumizi ya kuni na mkaa. Kwa kuwa sehemu ya kuni na mkaa unaotumika katika Jiji la Dar es Salaam huzalisha katika Wilaya ya Kibiti, hatua ya kuanza kutumia gesi asilia kwa kupikia itapunguza uharibifu mkubwa wa mazingira kupitia ukataji miti hovyo kwa matumizi ya kuni na mkaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hatua nyingine tarehe 18 Mei, 2018, Serikali kupitia Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) ilisaini kataba nakampuni ya Mihan Gas Limited kwa ajili ya kusambaza vifaa vya kupikia, mitungi ya gesi na majiko kwa kutumia liquidifies Petroleum Gas au gesi ya mitungi kwa watumishi wa umma na wananchi wengine. Mpango huo pia unalenga kupunguza matumizi ya mkaa na kuni.