Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 28 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 231 2019-05-15

Name

Dr. Jasmine Tiisekwa Bunga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Vyuo Vikuu

Primary Question

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:-

Barabara zinazotoka Kidiwa hadi Tandali, Daraja la Mgeta hadi Likuyu, Visomolo hadi Lusungi na Langali SACCOS hadi Shule ya Sekondari Langali Tarafa ya Mgeta Wilayani Mvomero zimejengwa kwa nguvu za wananchi, lakini bado hazipitiki kutokana na vikwazo vya miundombinu na madaraja:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara hizo ili kuondoa adha wanazopata wananchi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Jasmine T. Bunga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Kidiwa – Tandali – Maguruwe yenye urefu wa kilometa 13.8 imefanyiwa upembuzi yakinifu na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) na kubaini zinahitajika shilingi bilioni 2.81 kwa ajili ya matengenezo makubwa (Rehabilitation Works) kwa kiwango cha zege katika sehemu za maeneo ya milimani na ujenzi wa miundombinu ya madaraja. Serikali inaendelea na mpango wa kutafuta fedha kwa kizingatia uwingi wa fedha zinazohitajika.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali imetenga jumla ya shilingi milioni 34.6 kwa ajili ya matengenezo ya muda maalum (Periodical Maintenance) kwenye barabara za kibaoni – Lukuyu na barabara ya Visomoro – Bumu – Mwalazi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa daraja (vented drift) katika Mto Songa.