Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 27 Water and Irrigation Wizara ya Maji 227 2019-05-14

Name

Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE aliuliza:-

Benki ya Dunia imefadhili miradi ya visima kumi (10) katika kila wilaya nchini:-

Je, Serikali imefanya tathmini kujua asilimia ya miradi iliyofanikiwa na ambayo haikufanikiwa; na kwa ile ambayo haikufanikiwa, Serikali haioni haja ya kuingiza fedha ili kukamilisha miradi hiyo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vedasto Edgar Ngombale, Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2016, Wizara ya Maji ilifanya tathmini ya kina nchi nzima ili kujua idadi ya visima vyote vilivyochimbwa kwa Awamu ya Kwanza ya Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji katika Halmashauri zote Tanzania Bara. Idadi ya visima vilivyochimbwa ni 1,485. Kati ya hivyo, visima 990, sawa na asilimia 67 vilipata maji na visima 495 sawa na asilimia 33 vilikosa maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo ambayo visima vyake vilikosa maji Serikali ilitumia vyanzo vingine mbadala kama vile chemchemi, mito, maziwa au kujenga mabwawa ili kuhakikisha maeneo yaliyopewa kipaumbele katika mpango wa vijiji 10 yanapata huduma bora ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali imeanzisha Mfuko wa Maji wa Taifa ambao unalipa miradi yote iliyochelewa kukamilika na miradi mipya inayoendelea kujengwa katika Halmashauri zetu. Lengo ni kuhakikisha huduma bora ya maji kwa kila mwananchi.