Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 27 Water and Irrigation Wizara ya Maji 226 2019-05-14

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA Aliuliza:-

Serikali ilikopa fedha za mkopo nafuu kutoka Serikali ya India kwa ajili ya miradi 26 ya maji ikiwemo Mji wa Makambako.

Je, ni lini mradi huo wa maji utaanza na kukamilika?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI Alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, Mbunge wa Makambako kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imepata mkopo wenye masharti nafuu wa dola za Marekani milioni 500 kutoka Serikali ya India kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji katika miji 28 kwa upande wa Tanzania Bara na mradi mmoja upande wa Zanzibar. Utekelezaji wa miradi hiyo umegawanyika katika awamu mbili; awamu ya kwanza ni usanifu na awamu ya pili ni ujenzi wa miradi husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Wizara imefikia katika hatua za mwisho za kumpata mtaalam mshauri kwa ajili ya kuandaa ripoti (detailed project report). Baada ya ripoti ya mradi kukamilika, Wizara itaendelea na hatua ya kutafuta wakandarasi kwa ajili ya ujenzi wa miradi. Ujenzi wa miradi hiyo unatarajiwa kuanza katika mwaka wa fedha 2019/ 2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, muda wa kukamilika miradi hiyo utajulikana mara baada ya usanifu kukamilika.