Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 26 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 216 2019-05-13

Name

Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA Aliuliza:-

Miongoni mwa malengo ya Benki ya TPB ni kupeleka huduma ya kibenki kwenye maeneo ya vijijini na pembezoni ambayo hayafikiwi na huduma hizo:-

Je, ni kwa kiasi gani lengo hilo limefikiwa mpaka kufikia mwaka 2018?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Juma Othman Hija, Mbunge wa Tumbatu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, miongoni mwa malengo ya Benki ya TPB ni kupeleka huduma za kibenki na pembezoni mwa miji, kuongeza wigo na mtadao wa biashara ya benki ya kutumia teknolojia ya kisasa.

Katika kutekeleza malengo haya, Benki ya TPB imefanikiwa kuboresha huduma za kibenki kupitia mtandao wa ofisi 200 za Shirika la Posta Tanzania zilizopo katika kila wilaya na baadhi ya tarafa na kutumia teknolojia ya habari na mifumo ya kisasa kutoa huduma za kibenki ikiwemo simu za kiganjani (TPB POPOTE), mawakala wa kampuni za simu, mashine za POS pamoja na ATM katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, Benki ya TPB imefanikiwa pia kuongeza idadi ya matawi makubwa kutoka 30 kwa mwaka 2017 hadi 36 mwaka 2018 na matawi madogo
yaliyoongezeka kutoka 37 mwaka 2017 hadi kufikia 40 mwaka 2018. Idadi hii ya matawi inahusisha matawi ya iliyokuwa Benki ya Twiga na Benki ya Wanawake Tanzania. Matawi yote yameunganishwa kwenye mfumo wa TEHAMA unaowawezesha wateja kupata huduma za kibenki bila kutembelea matawi walipofungulia akaunti zao.

Mheshimiwa Spika, vituo vya huduma ndani ya Ofisi za Shirika la Posta viliongezeka kutoa 40 mwaka 2017 hadi kufikia 45 mwaka 2018. Aidha mashine za ATM ziliongezeka kutoka 51 mwaka 2017 hadi kufikia 72 mwaka 2018. Vilevile, mawakala wa SELCOM POS waliongezeka kutoka 225 kwa mwaka 2017 na kufikia 670 Desemba, 2018. Vituo vyote vua huduma ndani ya Ofisi za Shirika la Posta vimeunganishwa pia kwenye mtandao na mfumo wa TEHAMA wa benki na hivyo kutoa fursa kwa wateja wa vijijini na pembezoni mwa miji kupata huduma kwa wakati kama ilivyo kwa wateja wengine wanaohudumiwa na matawi makubwa na madogo.

Mheshimiwa Spika, jumla ya akaunti 227,052 zilifunguliwa na wananchi wa vijijini na pembezoni mwa miji kwa kutumia mfumo wa kutoa huduma za kibenki kwa njia ya simu za kiganjani, ujulikanao kama TPB POPOTE. Mfumo huu wa TPB POPOTE unasaidia wananchi kufanya malipo mbalimbali kama kuhamisha salio, kutuma fedha, kulipa ankala za maji, kununua umeme wa luku na kununua vocha za simu bila kulazimika kwenda katika matawi ya benki ya TPB. Wateja wanaweza pia kuhamisha salio kwenda katika akaunti nyingine, kuhamisha fedha kwenda katika akaunti zao za M-Pesa, Tigo Pesa, Airtel Money na Halopesa na hatimaye kuchukua fedha kupitia mawakala.